Topics
Wakati mwingine matumizi ya dawa kali au zenye sumu
huifanya damu kuwa na sumu.
Kutokana na hilo, vipele au madoadoa hujitokeza
mwilini, na wakati mwingine mtu hupata mizinga.
Athari ikiwa kali zaidi, mgonjwa huhisi maumivu ya
kuchoma kichwani na mwilini hupata degedege (spasms).
Wakati mwingine hupoteza fahamu.
Ikiwa damu imeathiriwa kutokana na Food Poisoning
au kuumwa na viumbe wenye sumu kama nyoka, nge, nyigu au nyuki, soma Matendo ya
Kiroho iliyotolewa katika kitabu na upulizie ndani ya maji.
Mnyweshe mgonjwa maji hayo.
Pia pulizia kwenye kipande cha udongo laini na umnusishe mgonjwa mara kwa mara.