Topics

Kuona Damu Ikielea Mbele ya Macho

 

Ugonjwa huu hutokea kutokana na kujaa maji ndani ya nyuzi za ubongo.

Kwa ajili yake, dawa na dua ni hii:

Chukua Pilipili nyekundu kiasi cha robo ratili moja na sukari kiasi cha robo ratili moja.

Visage vizuri katika kinu mpaka vipate kuwa unga laini.

Tumia kila siku kiasi cha gramu sita (6) wakati wa kulala pamoja na maji safi kwa angalau siku ishirini (20).

Pamoja na hayo andika:

اَلرَّضَاعَتْ عَمَا نَوِيلْ

Ar-Radaa'at Ama Naweel

juu ya sahani tatu nyeupe za kauri.

Asubuhi, jioni na usiku, osha sahani moja kwa maji na uyanywe maji hayo.

Njia ya kuandika sahani ni hii:

Weka mbele yako sahani tatu safi za kauri au kioo.

Soma mara kumi na moja (11):

يَا حَفِيظُ

Ya Hafeez

na pulizia juu ya sahani zote tatu.

Kisha soma mara kumi na moja (11):

يَا شَافِي
Ya Shaafee

na pulizia juu ya sahani zote tatu.

Mara ya tatu soma:

يَا كَافِي
Ya Kaafee

na pulizia juu ya sahani hizo.

Baada ya hapo changanya zafarani (saffron) katika maji ya waridi (rose water), au changanya rangi ya manjano ya chakula katika maji ya waridi, na kwa wino huo andika maneno yaliyotajwa hapo juu juu ya sahani.

Topics